Jumatano, 15 Machi 2017

Timu nane zilizofanikiwa kufuzu robo fainali ya UEFA Champions League 2016/2017

Usiku wa March 15 2017 ilichezwa michezo miwili ya mwisho ya hatua ya 16 bora ya marudiano ya michuano ya UEFA Champions League msimu wa 2016/2017, Man City walisafiri kucheza dhidi ya AS Monaco Ufaransa wakati Atletico Madrid walikuwa wenyeji wa Bayer Lerkusen ya Ujerumani.

Kwa bahati mbaya Man City wanaaga michuano hiyo kwa kukubali kipigo cha goli 3-1 hivyo wanaondolewa kwa aggregate ya 6-6 kutokana nakuruhusu kufungwa goli nyingi nyumbani, kwa upande wa Atletico Madrid wanafuzu kwa kuifunga Bayer
kwa aggregate ya goli 4-2 licha ya mchezo wa leo kumaliza kwa sare tasa 0-0.

Michezo hiyo ndio iliyofunga hatua ya 16 bora ya michuano ya UEFA Champions League msimu wa 2016/2017, kwa sasa michuano ya
Champions League inaingia hatua ya robo fainali, kufahamu timu ipi itacheza na ipi itajulikana Ijumaa ya March 17 baada ya kuchezeshwa droo.

By Thomas CEO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni